Mkazi wa Shikombe wilayani Geita, Buhula Ngassa (47) amekamatwa
na vitambulisho 43 vya wapiga kura, hata hivyo amedai vilikuwa vya
wateja wake waliofika kwake kusajili simu.
Kamanda wa
Polisi mkoa wa Geita, Joseph Konyo amesema leo kuwa mtuhumiwa Ngassa
alikutwa na vitambulisho vya zamani 7 na 36 ni vipya ambavyo
vitengenezwa kwa kutumia teknolojia ya BVR.
Kamanda
Konyo ameongeza mtuhumiwa amejitetea kuwa vitambulisho hivyo vilikuwa ni
kwa ajili ya kuwasajilia wateja waliofika kwake wakihitahitaji huduma
hiyo hivyo alikuwa anaenda maeneo ya mjini ili avidurufu na kupata
kumbukumbu atakazoziwasilisha kwa kampuni za simu.
Hata
hivyo RPC Konyo amesema uchunguzi zaidi unaendelea kubaini ukweli wa
sakata hilo. Awali, ilidaiwa kuwa mtuhumiwa alikamatwa na vitambulisho
200 vya kura lakini Jeshi la Polisi Geita limethibitisha kuwa ni 43
pekee.